• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wananchi watakiwa kulima alizeti

Posted on: July 16th, 2019

Wananchi watakiwa kulima alizeti 

Wananchi wa kijiji cha Mchinga II na wilaya ya Lindi wametakiwa kulima alizeti kwa wingi kwa kuwa soko la uhakika lipo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi wakati alipotembelea kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti kinachomilikiwa na kampuni ya Kilimo Timilifu (KT) ambacho kimejengwa katika kijiji cha Mchinga II wilayani Lindi.

Mhe. Zambi amesema ujenzi wa kiwanda hicho kunatoa fursa kwa wananchi kunufaika kupitia kilimo cha alizeti kwa kuwa soko la uhakika lipo. Kinachotakiwa ni wananchi kuwatumia KT na wataalam wa kilimo ili wawasaidie namna bora za kilimo hicho.

“Viongozi na wataalam wa kilimo ni lazima muanze sasa kuwaelimisha wananchi njia sahihi za kilimo cha alizeti na kuwahimiza waanzishe mashamba kwa kuwa soko lipo”, alisema Zambi.

Pia amewasihi wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki mafunzo yanayotolewa na kampuni KT ambao licha ya kutoa elimu ya kilimo cha alizeti kwa kuzingatia utunzaji wa mazingira, wanatoa elimu ya kilimo cha mbogamboga na ufugaji wa kuku. Hii ni kutokana na taarifa alizopewa kuwa wananchi hasa katika eneo la mradi kutojitokeza kikamilifu katika kujifunza.

Aidha, ameipongeza kampuni kwa uamuzi wake wa kuja kuwekeza kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti katika kijiji cha Mchinga II wilayani Lindi. Uwepo wa kiwanda hicho licha ya kutoa ajira kwa wananchi pia kitanunua  alizeti kwa wakulima, kununua kuku kutoka kwa wafugaji kwa ajili ya kuchinjwa katika machinjio iliyojengwa.

Akielezea shughuli za kampuni Katibu wa Kampuni, Mwassa Jingi amesema kampuni hiyo haina mmiliki bali inaongozwa na menejimenti kwa niaba ya wananchi na hupata msaada kutoka kwa wadau mbalimbali kwa ajili ya kukamilisha mradi ili waweze kuendesha shughuli zao wenyewe.

Jingi amemuomba Mkuu wa Mkoa na viongozi wengine kuendelea kuwahamasisha wananchi kwenda kujifunza kuhusu kilimo hifadhi na kulima alizeti kwa wingi. Hii itawezesha kiwanda hicho chenye mahitaji ya tani 250 kwa mwaka kufanya kazi mwaka mzima kwa kuwa na uhakika wa kupata malighafi za kutosha kwani wao hawatalima alizeti badala yake watategemea kupata kutoka kwa wananchi.

Pia amemuomba kupitia kwa maafisa maendeleo ya jamii na maafisa mifugo kuanza kuwahamasisha wananchi kujiandaa na ufugaji wa kuku ambao vifaranga vyake vitakuwa vikizalishwa na kituo cha KT ambavyo vinatarajiwa kati ya Octoba-Novemba, 2019 vitaanza kutoka.

Vilevile ameomba wataalam wa halmashauri kutoa ushirikiano pale taaluma zao zitakapohitajika kwani kwa udogo wa kampuni haitaweza kuajiri watu wote.

Naye mkuu wa wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga amesema wilaya tayari imeshapata wakulima zaidi ya 4,000 ambao itawatambua kwa kujua ukubwa wa mashamba waliyonayo. Pia kulikuwa na changamoto ya upatikanaji wa mbegu lakini kwa kushirikiana na Aghakhan Foundation na mradi wa Tilage watasambaza mbegu hizo za alizeti. Hivyo KT kwa kushirikiana na wataalam watasaidia kuwaongoza wananchi kuhusu namna bora za kilimo cha alizeti.

Mtendaji Mkuu wa kampuni ya KT, Timoth Tanner licha ya kumshukuru mkuu wa mkoa kwa kutembelea mradi, amesema nia ya mradi ni kuwasaidia wananchi wa hali ya chini kuondokana na umaskini kupitia kilimo hivyo shughuli wanazopanga kufanya zinahitaji ushiriki wa wananchi kikamilifu.

Ahmed Selemani, mwenyekiti wa kitongoji cha kijiji cha Mchinga II ameshukuru kwa ujenzi wa kiwanda kwani wananchi watapata ajira na sehemu ya kuuzia alizeti watakazokuwa wanalima. Pia wananchi watanufaika na elimu ya kilimo hifadhi, kilimo cha mbogamboga na ufugaji wa kuku ambapo machinjio yake itakuwa kiwandani.

Katika ziara hiyo mkuu wa mkoa Zambi alitembelea bustani inayotumika kufundishia kilimo cha mbogamboga na kukutana na akina mama wanaofundishwa, alitembelea shamba na kuona eneo lililolimwa kwa kuzingatia kilimo hifadhi, eneo la kiwanda cha alizeti ambacho kipo tayari na machinjio ya kuku ambayo ipo katika hatua za umaliziaji.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.