• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Watumishi watakiwa kufanya kazi kwa kujituma

Posted on: July 2nd, 2019

Watumishi watakiwa kufanya kazi kwa kujituma

Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Bi. Rehema Madenge amewataka watumishi wa ofisi ya mkuu wa mkoa kufanya kazi kwa kujituma na kuhakikisha wanatoa huduma bora.

Bi. Madenge aliyasema hayo wakati alipofanya kikao na watumishi hao kilichojadili masuala mbalimbali ya kiutendaji, na kiutumishi kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi na utoaji huduma bora kwa wateja. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa.

Watumishi wametakiwa kuacha tabia ya kufanya kazi kwa mazoea badala yake wafanye kazi kwa kujituma na kujitolea ili wateja wa ndani na nje ya ofisi waweze kupata huduma bora.

“Sote tunapaswa kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu, uadilifu, upendo, kuheshimiana na ushirikiano”, alisema Bi. Madenge. ‘Watumishi mnapaswa kuheshimiana licha ya kuwa na cheo kama zilivyo mila na desturi za watanzania’, aliongeza Bi. Madenge.

Aidha, watumishi wametakiwa kufuata miongozo mbalimbali ya kiutendaji inayotolewa ili kujiepusha na matatizo yanayoweza kuwapata kutokana na kutoifuata. Pia amewashukuru watumishi kwa mapokezi mazuri na ushirikiano waliompa tangu alipofika mkoa wa Lindi huku akiwasihi kuendelea na ushirikiano huo kwani ndio njia kubwa itakayoweza kuleta mafanikio.

Naye Katibu Tawala Msaidizi – Utawala na Utumishi, Dkt. Bora Haule alisema kuwa sehemu yake inaendelea kufanya maboresho kwa kuhakikisha stahiki za watumishi zinasimamiwa kwa mujibu wa taratibu na miongozo inayotolewa. Pia aliwasihi watumishi kuendelea kutoa taarifa pale wanapoona kuna tatizo ili waweze kupatiwa huduma kwa wakati.

Lucas Mbembela, Mchumi kutoka sehemu ya Serikali za Mitaa alisema kikao hicho kimetoa fursa kwa watumishi kujadili mambo mbalimbali zikiwemo changamoto wanazokutana nazo hivyo ni imani yake kuwa yale yote yaliyojadiliwa yatafanyiwa kazi.

Hawa Hatibu alisema kikao kama hicho kinasaidia kujadili mambo muhimu ya taasisi na kutoa fursa kwa watumishi katika ngazi zote kuweza kutoa malalamiko, maoni au ushauri lengo likiwa ni kuimarisha utoaji bora wa huduma kwa wateja wa ndani nan je.

Kikao cha watumishi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Lindi kimejadili mambo mbalimbali kiutendaji na kiutumishi kwa lengo la kuimarisha masuala ya kiutendaji na maslai ya watumishi lengo likiwa ni kuona namna ya kufanya maboresho katika utendaji na utoaji huduma kwenye mwaka huu mpya wa fedha 2019/2020.


PICHA MBALIMBALI ZA WATUMISHI WAKIWA KATIKA KIKAO

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.