• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

''WAZAZI SHIRIKIANENI NA WALIMU"- RC TELACK

Posted on: March 1st, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab R. Telack amewataka wazazi na walezi wa wanafunzi ndani ya mkoa wa Lindi kushirikiana na walimu katika kuhakikisha maendeleo ya kitaaluma na kinidhamu kwa wanafunzi na kubainisha kuwa ushirikiano huo utapunguza mzigo kwa walimu kitaaluma na kumfanya mzazi apate tathmini ya kile anachojifunza mtoto wake awapo shuleni.

Mhe. Telack ameyasema hayo katika hafla ya utoaji wa tuzo za kielimu iliyofanyika katika wilaya ya Kilwa, iliyoratibiwa na  ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Lindi na kuhudhuriwa na watumishi mbalimbali kuanzia ngazi ya Halmashauri, viongozi wa chama na serikali, walimu wa shule mbalimbali za umma na binafsi pamoja na wanafunzi.

“Wazazi wawafuatilie watoto wao na kutoa ushirikiano mzuri kwa walimu ili kupunguza mzigo katika malezi ya wanafunzi hawa wawapo katika mazingira ya shule, lakini pia mwanafunzi ana wajibu wa kusoma kwa bidii na kufanya tathimini ili kujua kile ambacho amejifunza darasani akiwa na mwalimu amekielewa kwa kiasi gani’’ amesema Mhe. Telack.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametoa pongezi kwa watumishi wote kuanzia ngazi za wilaya, halmashauri, walimu na wanafunzi kwa kazi nzuri iliyofanywa na kupelekea mkoa kushika nafasi ya 8 kitaifa kutoka nafasi ya 26 na kubaki katika nafasi ya kwanza kati ya mikoa miotatu iliyopandisha ufaulu wa wanafunzi kwa miaka mitatu mfululizo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Zainab R. Kawawa amewataka wanafunzi kutunza mazingira na miundombinu wanayoitumia kujifunzia ili iweze kuwanufaisha na wanafunzi wengine pale kipindi chao cha masomo kitakapo hitimika.

“Niwaombe wanafunzi muongeze bidii katika kujifunza, muongeze juhudi katika kuhudhuria masomo yenu na pia kutunza miundombinu yenu ya kujifunzia ikiwemo majengo, madawati na vitabu pia ili mkimaliza nyinyi vije viwanufaishe na wengine” amesema Mhe. Kawawa.

Hafla hiyo ilihusisha utoaji wa tuzo, vyeti vya pongezi na zawadi za pesa taslimu kwa halmashauri, walimu na wanafunzi walioibuka vinara katika matokeo ya kitaifa kwa lengo la kupongezana na kupeana motisha ya kuendelea kufanya vizuri zaidi ambapo pia zoezi hilo lilipambwa na burudani mbalimbali za mashairi, ngonjera, ngoma na nyimbo mbalimbali zilizoandaliwa na walimu pamoja na wanafunzi mbalimbali wa shule za msingi na sekondari.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.