• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WAZIRI AWESU APONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAJI LINDI

Posted on: September 20th, 2022

Waziri wa maji Mhe. Juma Awesu ametoa pongezi kwa viongozi na wasimamizi wa maji wa Mkoa wa Lindi kwa namna wanavyosimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji inayoendelea kutekelezwa  katika wilaya za mkoa wa lindi.

Waziri Awesu ametoa pongezi hizo jana alipofika na kufanya kikao kidogo  katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi  ambapo alipokea taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji inayotekelezwa mkoani Lindi, taarifa ambayo ilisomwa na Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Shaibu Ndemenga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.

“Nitumie nafasi hii kuwapongeza watendaji wetu kwa kazi kubwa wanayoifanya, utekelezaji wa miradi ya maji hauna sababu ya kuwa siri ,jamii ipo ukiishirikisha utafanikiwa, Luwasa ya Lindi mjini hongereni sana mnafaya kazi nzuri ” amesema Mhe. Awesu .

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji kwa upande wa Wilaya ya Lindi, Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Shaibu Ndemanga, amesema miradi mingi ipo kwenye utekelezwaji ambapo aliainisha baadhi ya miradi ambayo utelezwaji wake umekamilika kwa zaidi ya silimia 90%.

“ Tuna mradi wa maji maeneo ya Mitwero, Kitunda na Mkwaya maeneo ambayo yapo pembezoni na vyanzo vya maji………mwanzoni ilikuwa tuutekeleze kwa bilioni takribani 6.8, wenzetu hawa walikaa chini wakachambua wakasema tunaweza kufanya kwa force akaunti  ikashuka mpaka bilioni 3.6 kwa hiyo ule mradi umekamilika kwa asilimia  98% na tunatarajia kuukamilisha hivi karibuni, lakini pia tuna mradi wa Ng’apa, Kiduni ,Mayani na Ngongo wa milioni 608 ambao tumekamilisha kwa 100%  na maji yanatoka.”

Aidha Mhe. Ndemanga aliainisha miradi mingine inayoendelea ambayo ni miradi ya maji ya Mitwero Mchinga, Nyangao Mtama, pamoja na mradi wa Lindi Ruangwa ambao unafanyika ili kupeleka maji kutoka wilaya ya Lindi kwenda wilayani Ruangwa.

Waziri Awesu yupo ziarani mkoani Lindi kufuatilia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji katika Wilaya za Ruangwa na Liwale ambapo miradi hiyo inatekelezwa kwenye taasisi za VETA na vituo vya afya ili kuhakikisha taasisi hizo zinapata huduma hiyo.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.