• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WAZIRI JAFO ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA BANDARI YA UVUVI KILWA

Posted on: September 17th, 2024

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt Seleman Jafo ametembelea mradi wa Ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa juhudi za serikali za kuimarisha miundombinu ya sekta ya uvuvi nchini.


Ziara hiyo imekuja wakati utekelezaji wa ujenzi wa bandari hiyo ukiwa kwenye hatua muhimu, huku mradi huo ukitarajiwa kuleta mafanikio makubwa kwa wavuvi, jamii ya Kilwa na taifa  kwa ujumla.


Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Waziri Jafo ameeleza kuwa ameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo na kusisitiza kuhusu dhamira ya serikali ya awamu ya sita ya kuwekeza na kuboresha miundombinu muhimu ambayo itasaidia kukuza sekta ya uvuvi na biashara zinazohusiana na rasilimali  bahari.


"Ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa ni sehemu ya mpango mpana wa serikali wa kuboresha miundombinu ya kiuchumi, tukumbuke kuwa katika nchi, huu ni uwekezaji wa kwanza mkubwa katika bandari hii kubwa nzuri ya uvuvi ambayo itabadilisha kabisa uchumi wa taifa letu hili katika sekta ya uvuvi. Ndani ya muda mfupi tukumbuke Mhe. Rais ametoa Bil 266 kwa ajiri ya mradi huu na tunaona utekelezaji wake unakwenda vizuri." amesema Waziri Jafo.


Aidha, Mhe. Jafo ameongeza kuwa, bandari hiyo itasaidia kurahisisha shughuli za uvuvi huku ikifungua fursa za kibiashara kwa wananchi na kuongeza thamani ya mazao bahari hususan samaki, kufungua fursa za uwekezaji wa samaki kutokana na kusaidia upatikanaji wa malighafi kwa urahisi hivyo uchumi wa nchi kuendelea kujikita zaidi.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack ameishukuru serikali kwa uamuzi wa kuiwezesha Halmashauri ya Kilwa kuwa kitovu cha bandari ya kwanza ya uvuvi ya kisasa na kueleza kuwa fursa hiyo inakwenda kuwapatia wavuvi soko la uhakika la samaki wanaowavua pamoja na kuwawezesha wajasiriamali na wawekezaji kupata eneo maalumu la kupata malighafi.


Ziara ya Waziri wa Viwanda na Biashara katika ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa inaashiria hatua kubwa katika kuimarisha sekta ya uvuvi, ikifungua fursa za ajira na kuboresha maisha ya jamii ya wavuvi. Hii ni ishara ya uwekezaji endelevu wa serikali katika miundombinu na uchumi wa buluu kwa maendeleo ya taifa.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.