• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WAZIRI MKUU ASHUHUDIA UTIAJI SAINI MKATABA WA MRADI MKUBWA WA MAJI, LINDI

Posted on: February 18th, 2023

Leo Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameshuhudia utiaji saini mkataba wa ujenzi wa mradi wa maji Mkoani Lindi utakaonufaisha vijiji 34 vya Wilaya ya Ruangwa na Vijiji 21 vilivyopo Wilaya ya Nachingwea.

Hafla hiyo imefanyika Leo katika ukumbi wa Chuo cha Ufundi Stadi, VETA kilichopo kijiji cha Nandagala, Wilaya ya Ruangwa.

Mradi wa maji ambao umesainiwa Leo Kati ya Wakala wa Maji na Usafi Vijiji, RUWASA na Wakandarasi wawili wa ndani ambao ni M/STC Construction Company Limited  na M/S. Emirates Builders Construction Limited unaenda kupunguza kwa kiasi kikubwa cha changamoto ya upatikanaji maji Safi na salama kwa wananchi wa Wilaya za Nachingwea na Ruangwa.

Mradi huo mkubwa wenye thamani ya Tsh. bilioni 119.15 ni moja ya Miradi michache mikubwa inayotekelezwa na wakandasi wa kitanzania.

Akizungumza mbele ya wananchi wa Ruangwa, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema kuwa mradi huu ambao utaanzia kwenye chanzo cha maji kilichopo kijiji cha Nyangao , Wilaya ya Lindi utatekelezwa na Wakandarasi wawili ili kuharakisha upatikanaji wa huduma ya maji Safi na salama kwa wananchi wa Ruangwa na Nachingwea ndani ya muda mfupi.

Mhe. Majaliwa Ameipongeza Wakala wa Maji  na Usafi wa Mazingira Vijijini, RUWASA kwa kufanikisha kila kjiji cha Wilaya ya Ruangwa kupata kisima cha maji ingawa changamoto kuwa maji ya visima hivyo yana chumvi. Hivyo kukamilika kwa mradi huu utaondoa kadhia ya wananchi kuzunguka na baiskeli, boda boda kutafuta maji yasiyo na chumvi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA, Ndg. Clement Kivegalo amewaeleza wananchi kuwa mradi huo unaotoka kwenye chanzo cha maji cha uhakika utakapokamilika utafikia lengo la kitaifa la upatikanaji wa maji Safi na salama kwa asilimia 85.

Ndg. Kivegalo ameendelea kusema kuwa kutokana na uwepo wa maji ya kutosha kwenye chanzo kilichopo katika kijiji cha Nyangao, mradi huu utaweza kuduma zaidi ya miaka 20.

Kwa upande wao, wananchi wa Ruangwa akiwemo Mariam Hamisi Chitanda kutoka kijiji cha Namahema, Wilaya ya Ruangwa wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha mradi huu mkubwa utakaoondoa changamoto ya ndoa nyingi kuvunjika Kwa sababu ya kutafuta maji.

Wananchi hao wameongeza kuwa kwa furaha waliyonayo wako tayari kujitolea kufanikisha ujenzi wa mradi huo kuanzia hatua ya mwanzo mpaka kukamilika kwake.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.