• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WIZARA YA SHERIA NA KATIBA YATOA MAFUNZO KWA WATAALAM WASHIRIKI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPGAIN MKOANI LINDI

Posted on: February 18th, 2025

Wizara ya Sheria na Katiba imeendesha kikao cha mafunzo na Wataalam wataoshiriki katika utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria Mkoani Lindi kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campgain) yenye lengo la kutoa elimu mbalimbali za Kisheria pamoja na utatuzi wa migogoro.


Akifungua kikao hicho kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Bwana. Nathalis Linuma ametoa rai kwa washiriki wa kikao hicho kuzingatia na kutumia mafunzo hayo kama chachu na mwangaza wa kuwasaidia wananchi kwa kuwapatia huduma za msaada wa kisheria katika kipindi cha kampeni.


"Ni matarajio yangu kuwa mtafata mwongozo wa utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia utakaotolewa na wataalam wa Wizara ili kuhakikisha kampeni inawanufaisha walengwa hususan wananchi wasio na uwezo wa kumudu gharama za Mawakili, ni vyema kuhakikisha kila mwananchi anaguswa na kampeni hii ili kwa pamoja tuweze kupunguza na kuondoa migogoro hususan ya kisheria inayowakabili wananchi"  


Aidha, Bwana. Linuma amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika maeneo ya mikutano ili waweze kupata fursa ya kujifunza kuhusu masuala ya kisheria na kupata nafasi ya kuwasilisha mashauri yao ya kisheria ili kupata ufumbuzi na utatuzi wa shauri husika kwa usahihi.


Kwa upande wake Mkurugenzi na Msajiri wa Watoa Huduma za Kisheria Bi. Ester Msambazi  ameeleza kuwa Kampeni hii inatekelezwa katika Mikoa  26 yaTanzania bara na 5 ya Tanzania visiwani ambapo kati ya hiyo Mikoa 17 tayari imeshafikiwa.



"Uwepo wa kampeni hii umetokana na ombwe kubwa la kisheria lililopo miongoni mwa wanajamii hivyo kampeni imekuja kuleta uelewa wa masuala ya kisheria na elimu ya sheria miongoni mwa wananchi pamoja na kutoa huduma ya msaada wa kisheria inayohusu usuluishi nanutatuzi wa migogoro ikiwemo ya ardhi, jinai na madai pamoja na masuala ya mirathi na wosia"


Msaidizi Msaidizi wa Jeshi la Polisi na Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Lindi, Joyce Kitesho ameeleza kuwa wanatarajia kampeni hii itakua ni chachu ya kupunguza migogoro mingi inayotokana na ukatili wa kijinsia ambayo waathirika wake wakuu ni wanawake na watoto kutokana na ukosefu wa elimu ya kisheria kunakopelekea waathirika kukosa haki zao panapotokea migogoro.


Kampeni ya Utoaji wa Huduma ya Msaada wa Kisheria itaendeshwa kwa muda wa siku 9 katika Halmashauri zote za Mkoa wa Lindi kuanzia Februari 19 hadi Februari 28, 2025 ambapo elimu mbalimbali zinazohusu masuala ya Haki za Binadamu na Utawala Bora pamoja na utatuzi wa migogoro ikiwemo ya ardhi, mirathi, wosia, madai na jinai zitatolewa.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.