• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

DC Nachingwea apewa maelekezo akiapishwa

Posted on: October 22nd, 2019

DC Nachingwea apewa maelekezo akiapishwa

Mkuu wa wilaya ya Nachingwea, Hashim Abdallah Komba amepewa maelekezo 11 ya kwenda kuyafanyia kazi mara baada ya kuapishwa.

Maelekezo hayo yalitolewa na mkuu wa mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi baada ya kumuapisha mkuu huyo wa wilaya, tukio ambalo lilifanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa na kushuhudiwa na wakuu wa wilaya, kamati ya ulinzi ya mkoa, wakurugenzi wa halmashauri, viongozi wa dini na watumishi wa sekretarieti ya mkoa wa Lindi.

Zambi amemtaka mkuu huyo wa wilaya licha ya kutimiza majukumu yake kuhakikisha kwanza wilaya ya Nachingwea vizuri kwa haraka. Pia ahakikishe anaboresha mahusiano kati ya ofisi ya mkuu wa wilaya na ofisi ya mkurugenzi.

Maagizo mengine ni kusimamia ukamilishaji wa ukarabati wa soko ambalo lililalamikiwa na wananchi wakati wa ziara ya Rais Magufuli, kusimamia ujenzi wa mabweni Nachingwea high school, kuhakikisha mabasi yote yanahamia stand mpya na kuhakikisha miundombinu inaendelea kuboreshwa huku halmashauri ikitakiwa kulipangia matumizi eneo lililokuwa la stand ya zamani.

Pia amemtaka kutatua migogoro ya ardhi iliyopo ambapo aliutaja mgogoro wa viwanja katika eneo la Namatula, kusimamia utoaji wa vitambulisho vya wajasiriamali, kusimamia zoezi la usafi wa mazingira sambamba na ujenzi wa vyoo. Na kuhakikisha amani na utulivu inatawala katika kipindi chote cha kampeni na uchaguzi wa serikali za mitaa.

Vilevile Zambi amewaagiza wakuu wa wilaya kusimamia miradi ya ujenzi hasa katika miundombinu ya afya na elimu. Mkuu wa mkoa amewaagiza kusimamia matumizi ya POS kwa kujua idadi yake, ngapi zinazofanya kazi, mahitaji halisi katika halmashauri na nini kinafanyika ili kuhakikisha fedha zinakusanywa kwa kutumia mfumo. Katika hili mkuu wa mkoa Zambi amehitaji kupata taarifa kabla au ifikapo tarehe 30 Oktoba, 2019.

Akizungumza baada ya kuapishwa, Mhe. Komba ameahidi kwenda kutimiza majukumu yake pamoja na maelekezo yote aliyopewa na mkuu wa mkoa. Pia amewaomba wananachingwea kumpa ushirikiano kwani kupitia ushirikiano ndio wataweza kukuza maendeleo ya Nachingwea.

Katibu Tawala Mkoa, Bi. Rehema Madenge aliwasihi viongozi na watumishi wote kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kama majukumu yao yanavyowataka ili kuhakikisha wanatoa huduma sahihi na kwa wakati kwa wananchi na kuhakikisha mkoa unasonga mbele kimaendeleo.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.