• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Zambi azuia uchimbaji wa dhahabu wilayani Nachingwea

Posted on: April 7th, 2020

Zambi azuia uchimbaji wa dhahabu wilayani Nachingwea

Mkuu wa mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi amezuia uchimbaji wa dhahabu katika kijiji cha Mpiruka B wilayani Nachingwea.

Akitoa ufafanuzi wa hali ya eneo hilo, mkuu wa wilaya ya Nachingwea, Hashim Komba alisema walibaini kuwa eneo hilo linachangamoto nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa vibali halali vya uchimbaji, wachimbaji kutokubaliana na mmiliki wa eneo hilo ambaye amelima mazao, kukosa vyoo, hakuna makusanyo yoyote ya serikali, na kulikuwa na ajira za watoto.

Lakini baada uongozi wa wilaya kuzungumza na wataalam wa madini walibaini kuwa eneo hilo lina leseni ya utafiti wa madini aina ya kinywe (graphite) ambayo illitolewa mwaka 2017. Wachimbaji wadogo wanalitumia eneo hilo kwa kuchimba dhahabu.

Kutokana na mapungufu hayo, mkuu wa mkoa Zambi aliwaeleza wachimbaji pamoja na wanakijiji kuwa amezuia uchimbaji huo kuanzia sasa mpaka hapo taratibu zinazotakiwa kufuatwa zitakapokamilishwa.

“Nauagiza uongozi wa wilaya uhakikishe unafunga shughuli zote za uchimbaji katika eneo hili mpaka hapo taratibu husika zitakapo kamilishwa” alisema Mhe. Zambi.

Aidha, mkuu wa mkoa Zambi amewataka wachimbaji wote ambao wametoka nje ya kijiji hicho kurudi kwao kwa kuwa kukamilika kwa taratibu hizo kutachukua muda wa zaidi ya miezi mitatu, na kwamba eneo hilo kwa sasa halitakiwi kufanyiwa uchimbaji kutokana na uwepo wa mazao yaliyopandwa na wamiliki hivyo ni lazima wasuburi kwanza mpaka wavune.

Pia ameuagiza uongozi wa wilaya kwa kushirikiana na kamishna wa madini kuhakikisha wanasimamia vizuri zoezi la fidia ili wananchi wanaomiliki maeneo hayo wapate haki yao. Hii ni pamoja na kuwasaidia wachimbaji hao wadogo na serikali ya kijiji kuweza kukamilisha taratibu zinazotakiwa ili shughuli za uchimbaji ziweze kuendelea hapo baadae.

Naye mmoja wa wamiliki wa maeneo hayo Bi. Zainabu Ng’ombo ameshukuru serikali kwa hatua zilizochukiliwa na viongozi za kusimamisha shughuli za uchimbaji. Bi. Ng’ombo amesema wachimbaji walikuta amepanda mazao yake kwa ajili ya chakula lakini walianza kuyang’oa wakati wakichimba madini na hivyo kusababisha uharibifu mkubwa. Pia aliomba kama taratibu zitakamilika kwa wakati ni vema uthamini wa maeneo hayo ukafanyika ili wamiliki walipwe haki yao ambayo itawasaidia kuondokana na usumbufu wanaokutana nao.

 Henrick Mustamba ambaye ni dereva bodaboda alisema uwepo wa wachimbaji hao ulikuwa ni fursa kwao kwani walikuwa wakiwabeba kila siku kuwapeleka machimbo kwa gharama y ash. 5,000. Pia walikuwa wakiuza maji kwenye madumu kitu ambacho kilikuwa kikiwaongezea kipato huku dumu moja la maji wakiuza kw ash. 1,500. Hivyo ameomba taratibu zinazohitajika kufanywa zifanyike kwa wakati ili shughuli hizo ziendelee.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.