• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

EQUIP

Start Date: 2015-03-01
End Date: 2018-03-01

EQUIP Tanzania

Mpango wa Kuboresha Elimu Tanzania (EQUI-  Tanzania) unafadhiliwa na serikali ya Uingereza kupitia mfuko wa maendeleo wa Uingereza, DFID. Mpango huu ni wa miaka minne ambao umeanza utekelezaji mwaka 2014 katika mikoa mitano hapa Tanzania yaani Dodoma, Kigoma, Shinyanga, Simiyu na Tabora na ikaongezwa mikoa ya Lindi na Mara mwaka 2015. Jumla ya fedha Tsh 136 bilioni zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huu kwa kipindi cha miaka minne.

Mpango huu unalenga kuongeza ubora wa elimu kwa shule za msingi unaozingatia jinsia. Mpango wa Kuboresha Elimu Tanzania unatarajia kuwafikia zaidi ya wanafunzi milioni mbili na zaidi ya walimu 49,000 waliopo shule 4,452, kata 1,123 zilizopo kwenye halmashauri 51 ndani ya mikoa saba ya mpango huu.

Katika ngazi ya mkoa mpango huu unasimamiwa na Katibu Tawala wa mkoa akisaidiwa na watendaji wa sekretarieti ya mkoa. Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ndiye msimamizi mkuu wa utekelezaji wa mpango wa uboreshaji wa elimu katika ngazi ya halmashauri. Hivyo watendaji wa halmashauri, waratibu elimu kata na walimu wakuu ndiyo watekelezaji wa shughuli zilizopangwa katika program hii kwa kushirikiana na wazazi na asasi za kiraia.

Katika kufikia maono ya Taifa ya kuboresha elimu Tanzania, EQUIP- Tanzania ina malengo makuu yafuatayo:

  • Kuongeza umahiri wa ufundishaji wa walimu kwa kuongezeka maarifa, ujuzi na ari katika utendaji kazi
  • Kuongeza umahiri katika usimamizi wa shule   
  • Kuongeza umahiri katika usimamizi wa elimu katika Wilaya na mkoa.
  • Kuongeza ushirikishwaji wa jamii katika elimu
  • Kuimarisha mfumo wa ukusanyaji taarifa, utunzaji na uwajibikaji
  • Mkoa wa Lindi ulianza kutekeleza program ya EQUIP-Tanzania mwezi Machi, 2015 na hadi sasa taarifa zifuatazo ndizo zinazotumika katika kupanga matumizi ya fedha kwa shughuli zilizopangwa.
  • Shughuli zifuatazo zimetekelezwa

    • Na
    • Halmashauri
    • Idadi ya shule
    • Idadi ya Kata za kielimu
    • 1
    • Kilwa
    • 108
    • 23
    • 2
    • Lindi Manispaa
    • 31
    • 10
    • 3
    • Lindi Vijijini
    • 117
    • 31
    • 4
    • Nachingwea
    • 105
    • 33
    • 5
    • Liwale
    • 55
    • 20
    • 6
    • Ruangwa
    • 82
    • 22
    • Jumla
    • 498
    • 139

    1. Katika kufikia lengo la kuongeza umahiri wa ufundishaji wa walimu darasani kwa kuongezeka maarifa, ujuzi na ari katika utendaji kazi walimu wamewezeshwa katika yafuatayo;
  • - Pia walimu wote wamepata ujuzi na maarifa ya jinsi ya kulitawala darasa wakati wa ufundishaji kwa kuzingatia jinsia (Gender Responsiveness).

    Wasimamizi wakuu wa mafunzo haya ni wahadhiri wa chuo kikuu huria Tanzania na Taasisi ya Elimu Tanzania. Serikali inategemea kuwa wanafunzi wa darasa na kwanza na la pili wajengewe uwezo wa kusoma, kuandika na kuhesabu kwa ufasaha kabla hawajaingia darasa la tatu.

    - Walimu wote wameweza kupata mafunzo ya jinsi ya kumfundisha mtoto/mwanafunzi jinsi ya kusoma, kuandika na kuhesabu. Mafunzo haya yamewezeshwa na wakufunzi toka vyuo vya ualimu Nachingwea, Mtwara na Kitangali.

    1. Kuongeza umahiri katika kuongoza na kusimamia shule: Katika eneo hili walengwa wakuu ni walimu wakuu na waratibu elimu kata.
  •        EQUIP -Tanzania.

     Pia wamefundishwa jinsi ya kutumia fedha ya ruzuku ya pikipiki ambayo wanapewa kila mwezi fedha zisizozidi Tsh 210,000 kwa ajili ya matengenezo ya pikipiki, mafuta na utawala akiwa kazini. Ni imani ya serikali kuwa walimu wakuu watakuwa mahiri katika kuongoza shule na waratibu elimu kata watasimamia kwa ukaribu shule zilizopo kwenye kata zao kwa kutumia uwezeshwaji uliofanywa na serikali chini ya program ya

     Waratibu elimu kata wamepewa mafunzo ya jinsi ya kutumia pikipiki walizokabidhiwa na serikali kwa ajili ya kusimamia shughuli za elimu katika kata zao.

     Mpango wa EQUIP-Tanzania umewawezesha kutambua sifa za shule mahiri, mwalimu mkuu/mratibu elimu kata mahiri, umahiri wa jinsi ya kuandaa mpango mkakati wa maendeleo ya shule, jinsi ya kuandika andiko mradi kwa maendeleo ya shule, umuhimu na kazi ya kamati ya shule, jinsi ya kuendesha kikao cha walimu cha kila wiki, na usimamizi na uongozi wa shule.

    1. Kuongeza umahiri katika usimamizi na uwajibikaji kwa wasimamizi wa elimu ngazi ya wilaya na mkoa katika kupanga na kusimamia shughuli za elimu. Viongozi wasimamizi wa elimu ngazi ya mkoa na wilaya ni wadau wakubwa katika kupanga na kusimamia utekeleza wa shughuli za elimu katika maeneo yao. Miongoni mwa yaliyotekelezwa ni;
  • Viongozi hawa pia wamehusishwa kwenye mafunzo mengi ambayo yamewezeshwa kwa walimu ili wapate uelewa wa shughuli zinazofanyika na wazisimamie kwa ufanisi mkubwa. Wakurugenzi na wahasibu wamewezeshwa kwenye eneo la usimamizi wa fedha na kutoa ripoti ya matumizi ya fedha kila mwezi na kila muhula. Serikali inauhakika shughuli zote zilizopangwa kwenye program ya EQUIP-Tanzania zitasimamiwa vizuri na mkoa husika.

    Viongozi wa mkoa wakiwemo katibu tawala wa mkoa, maafisa mipango, wakurugenzi, wahasibu, wakaguzi wa mahesabu wa ndani, maafisa maendeleo, maafisa elimu, wamewezesha kwa kupata mafunzo ya jinsi ya kuandaa mpango mkakati wa mkoa na wilaya kwa kuipa elimu kipaumbele kama dira ya maendeleo ya Taifa 2025 inavyoelekeza.

    1. Kuongeza ushirikishwaji wa jamii katika elimu: Jamii inayoizunguka shule inapaswa ijue kuwa shule ni mali yao kwa maana watoto wanaosoma wanatokea kwenye jamii hiyo. Pia miundombinu ya shule ipo kwenye maeneo yao, na kwa maeneo mengi shule hizo zimejengwa kwa nguvu za wananchi. Hivyo maendeleo yote katika shule ni faida kwa jamii husika. Miongoni mwa mafanikio katika ushirikishwaji wa jamii ni pamoja na;
  • Pia shule imepewa mbao ya matangazo ambapo shughuli zinazoendeshwa shuleni ziwe wazi kwa wananchi. Kwa ushirikiano huu ni imani ya serikali kwamba jamii zitakuwa karibu na shule kwa maendeleo ya jamii husika

    Kila Halmashauri imetengewa Tsh 10 million kwa muhula ili kusambaza taarifa za mafanikio kwa njia ya simulizi kwa jamii inayoizunguka.

    Nusu ya idadi ya shule za mkoa wa Lindi watapokea Tsh 1,500,000 kila shule kwa ajili ya kuendesha shughuli za uzalishaji ili kuitegemeza shule na wanafunzi wajifunze elimu ya kujitegemea. Hivyo shule itakuwa na miradi ya uzalishaji inayoongozwa na wanafunzi, walimu na jamii.

    Pia kila shule imeunda umoja wa wazazi na walimu ambapo kila darasa limewakilishwa na wazazi wawili wenye watoto katika darasa husika. Hivyo wazazi hao watakuwa wafuatiliaji wa karibu kwa kila siku katika darasa husika. Umoja huu umewezeshwa kiasi cha shilingi 550,000 kwa ajili ya shughuli za maendeleo na uhamasishaji kwa wanafunzi juu ya kujifunza. kamati za shule zimepewa mafunzo ya jinsi ya kusimamia shule kwa ukaribu na umuhimu wa uwepo wao kisheria.

    Mpango wa EQUIP- Tanzania umewezesha jamii kuelewa na kujenga uwezo wa kuwa na mipango ya kuisaidia shule kutatua changamoto mbalimbali watakazozibaini kwa kushirikiana na uongozi wa shule. Kwa kutumia Asasi za Kiraia, kila kijiji kimeunda kikosi kazi cha kusimamia katika kupanga na kutekeleza vipaumbele vya elimu katika maeneo yao.

      • Kuimarisha mfumo wa ukusanyaji taarifa, utunzaji na uwajibikaji: Taarifa za elimu ni muhimu sana kwa matumizi mbalimbali. Mpango wa EQUIP- Tanzania umewezesha kuboresha utaratibu wa kukusanya, kuhifadhi na kuzipata taarifa mbalimbali za elimu kutoka shuleni kwa urahisi na kwa matumizi yanayotarajiwa.
      • Waalimu wakuu na waratibu elimu kata wamewezeshwa mafunzo jinsi ya kukusanya na kuingiza taarifa hizo kwa kutumia vishikwambi ambapo walimu wakuu wote na waratibu elimu kata wote wamepewa vishikwambi vyenye mfumo maalumu wa ukusanyaji na utunzaji wa taarifa za elimu. Serikali chini ya ofisi ya Raisi TAMISEMI inaratibu mafunzo na kusimamia mfumo huu. Ni malengo ya serikali shule zote Tanzania zitumie mfumo huu kwa nyakati za usoni.
      • Tokea mwezi Machi, 2015 hadi Februari 2017 Serikali ya Uingereza imeshatuma fedha kwenye akaunti za maendeleo za halmashauri zetu kama taarifa inavyoonesha hapo chini
    • SN

      LGA

      1st,Tranhe

       2nd,Tranche 

       3rd,Tranche 

      4th,Tranche

      Total

      1

      Liwale DC
          265,078,388
          295,582,575
          231,382,549
          235,001,007
         1,027,044,519

      2

      Lindi DC
          500,521,416
          554,689,963
          429,782,548
          399,705,583
         1,884,699,510

      3

      Lindi MC
          163,446,185
          181,924,440
          127,861,929
          147,778,768
           621,011,322

      4

      Ruangwa DC
          396,915,485
          447,935,205
          310,281,619
          297,803,483
         1,452,935,792

      5

      Nachingwea DC
          465,642,421
          519,689,963
          407,064,744
          377,716,595
         1,770,113,723

      6

      Kilwa DC
          458,326,867
          511,356,233
          376,636,811
          356,018,852
         1,702,338,763

      7








      JUMLA KUU
       2,249,930,762 
        2,511,178,379 
       1,883,010,200 
       1,814,024,288 
         8,458,143,629 
      • Fedha hizi zimepangiwa kazi elekezi kwa walengwa waliopangwa kwenye mpango kazi wa kila halmashauri husika. Fedha zote zinatumika kuendesha mafunzo kwa waratibu elimu kata, walimu wakuu, walimu wa darasani ili kuwajengea uwezo katika nyanja mbalimbali na pia kuenga uwezo kwa jamii katika kupanga vipaumbele vya kuboresha elimu katika maeneo yao. Walimu wote wanatarajiwa kuwa mahiri katika uongozi, usimamizi na ufundishaji darasani ambapo mwanafunzi atapata mazingira bora ya kujifunza na kufundishwa vizuri akiwa darasani na hata nje ya darasa.
      • Kwa maelezo hayo hapo juu serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania inatumaini utekelezaji mahiri wa shughuli za mpango huu katika halmashauri za mkoa wa Lindi na usimamizi mzuri wa viongozi wa mkoa na wilaya utasaidia kutatua changamoto nyingi zinazotokana na umahiri wa utendaji wa wahusika na kuleta tija katika ubora wa elimu kwa shule za msingi. Pia uongozi wa program ya EQUIP - Tanzania unaomba uongozi wa serikali ngazi ya mkoa na wilaya kusimamia kwa karibu katika utekelezaji wa program hii ili uwekezaji mkubwa uliofanya na serikali ya Uingereza na Tanzania uzae matunda yaliyotarajiwa kwa kipindi husika. Wazazi na wadau wengine wa elimu tushirikiane na uongozi wa shule katika kutekeleza mipango shirikishi ya maendeleo ya shule zetu kwa manufaa ya Taifa la kesho (watoto).

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.